Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, ametangaza kuwa mazungumzo kati ya Iran na Marekani yatarejelewa mjini Geneva kwa kuzingatia makubaliano ya duru zilizopita. Amesema Tehran ina dhamira ya dhati ya kufikia makubaliano ya haki kwa muda mfupi iwezekanavyo.
Iran imesisitiza kuwa haitafuti kamwe silaha za nyuklia, lakini haitarudi nyuma katika haki yake ya kutumia teknolojia ya nyuklia kwa madhumuni ya amani.
Araghchi ameeleza kipindi hiki kuwa ni “fursa ya kihistoria” ya kuondoa wasiwasi wa pande zote mbili, akisisitiza kuwa kufikiwa kwa makubaliano kunawezekana tu kwa kuipa diplomasia kipaumbele.
Your Comment